Majukumu ya Bodi ya Mfuko ya Mfuko

Majukumu ya Bodi yameainishwa chini ya Kanuni ya 9 ya Kanuni za Mfuko wa Taifa wa Maji, Tangazo la Serikali Na. 981 la mwaka 2019.

Majukumu hayo yanajumuisha, lakini hayajaishia hapo, yafuatayo:

(a) kuhakikisha ukusanyaji kamili na uhamishaji wa fedha kutoka vyanzo mbalimbali kwenda kwenye akaunti ya Mfuko;

(b) kuhakikisha kuwa fedha zinazowekwa katika Mfuko zinatumika kufikia malengo ya Mfuko;

(c) kutoa fedha kutoka kwenye Mfuko kwa taasisi/waendaji wa utekelezaji kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji iliyoidhinishwa;

(d) kuhakikisha kuwa shughuli za Mfuko zinaendeshwa kwa njia ya kiuchumi na yenye ufanisi;

(e) kupendekeza kwa mamlaka husika kuchukuliwa kwa hatua stahiki dhidi ya matumizi mabaya ya fedha yanayofanywa na taasisi za utekelezaji;

(f) kuidhinisha makadirio ya mwaka ya mapato na matumizi na kuzingatia makadirio hayo;

(g) kusaini mikataba ya utendaji ya mwaka na taasisi za utekelezaji zinazopokea fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji;

(h) kuidhinisha orodha ya miradi yote inayofadhiliwa kwa kila robo mwaka na kuiwasilisha kwa Waziri kwa taarifa;

(i) kumshauri Waziri kuhusu matumizi na usimamizi wa fedha; na

(j) kumshauri Waziri kuhusu vyanzo vipya vya fedha kwa madhumuni ya kuhakikisha upatikanaji wa fedha wa kutosha na endelevu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji.