Kikao Matumizi ya TEHAMA katika Sekta ya Maji
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb), na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki (Mb),katika kikao majadiliano kuhusu kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika Sekta ya Maji kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Kikao hicho kimejikita katika mageuzi ya kidigitali yatakayosaidia kuongeza ufanisi, kudhibiti upotevu wa maji na mapato, pamoja na kuboresha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kisasa ya kiteknolojia. Kikao kilifanyika jana, Februari 2, 2026, Mtumba, Dodoma.